Sehemu ya Upasuaji wa Macho

Idara ya Magonjwa ya Macho ilianza kutoa huduma kwa wananchi wenye matatizo ya macho mnamo oktoba, 2015 kwa kutoa huduma za kliniki pekee.

Kwa wakati huo 2015, Idara ya Magonjwa ya macho iliendeshwa na Muuguzi mmoja wa macho, pamoja na daktari bingwa wa macho. 

Baadae, idara ya Magonjwa ya macho iliongeza muuguzi msaidizi wa macho na kuiwezesha kufanya huduma-mkoba iliyofadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali, huduma hiyo ilisababisha idara ya macho kufahamika miongoni mwa wananchi.

Baada ya huduma-mkoba kuitambulisha Idara ya Magonjwa ya macho, ikiwa ni pamoja na kupata ufadhili wa vifaa vichache kutoka kwa wadau  hao, Idara iliweza kuongeza huduma na kuanza kufanya upasuji mdogo.

Mnamo mwaka 2018, Idara ya Magonjwa ya Macho ilipata Madaktari wengine wawili, hivyo kufanya idadi ya watumishi katika idara hiyo kuwa watano (05).

Baada ongezeko la watumishi idara ilifanikiwa pia kupata Hadubini yenye uwezo wa kufanya uchunguzi na matibu (operating microscope) inayotumika hadi sasa.

Kwa bahati nzuri, shirika lingine lisilokuwa la kiserikali (NGO) lijulikanalo kama KCCO liliamua kufadhili huduma-mkoba kwa wagojwa wenye mtoto wa jicho, na kwa sababu hiyo, walinunua Hadubini nyingine yenye uwezo wa kuchunguza na kutibu.

Kuanzia mwaka 2019, Idara ya magonjwa ya macho imekuwa ikikua siku hadi siku, kufikia idadi ya manesi wawili wa macho, Madaktari wa macho wawili, Muuguzi msaidizi mmoja, Meneja wa Huduma Mkoba mmoja, na mtoa huduma za jamii mmoja.

Dondoo za Afya na Habari
Kula Mlo Kamili
Kula Mlo Kamili

Eat a combination of different foods, including fruit, vegetables, legumes, nuts and whole grains. A...

  View more
Usivute Sigara
Usivute Sigara

Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mapafu yako, uvutaji wa sigara unaweza sababisha matatizo ya...

  View more
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta

Fats consumed should be less than 30% of your total energy intake. This will help prevent unhealthy...

  View more
Kuendesha Gari.
Kuendesha Gari.

Unashauriwa kutokuendesha gari kila siku na wakati mwingine unatakiwa kutembea walau miguu yako na m...

  View more
Epuka ulevi wa Pombe
Epuka ulevi wa Pombe

There is no safe level for drinking alcohol. Consuming alcohol can lead to health problems such...

  View more