BMH YASIFIWA KWA KUTUNZA MAZINGIRA
BMH YASIFIWA KWA KUTUNZA MAZINGIRA

Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano), Bi Marry Maganga, ameisifia Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kwa kutunza mazingira vizuri hivyo kufanya eneo linalozunguka hospitalini hapo kuwa salama.

Bi Maganga ametoa sifa hizo wakati alipotembelea hospitalini hapo mwisho wa mwezi Mei wakati wa Wiki ya Mazingira, akisema Serikali itaitumia Hospitali hiyo ya Rufaa ya Kanda ya Kati kama rejea ya Utunzanzaji Mazingira.

“Tunajivunia kuwa na taasisi (BMH) inayotunza mazingira vizuri, yenye mfumo mzuri wa kutibu majitaka…Nawapongeza BMH,” alisema Katibu Mkuu baada ya kutembelea Hospitali hiyo ya Umma na kupanda mti katika eneo la Hospitali.

Bi Maganga ameagiza uongozo wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kulinda eneo la BMH la kutibu majitaka ili watu watu wenye tabia ya kuvamia maeneo wasiweze kulivamia eneo hilo kwa sababu mji unakua kwa kasi.

“Hii inatuonyesha kuwa tupo salama tunapopata huduma za afya hapa Hospitali ya Benjamin Mkapa.Kutoka jikoni mpaka kantini, mazingira ni safi,” alisema Katibu Mkuu.

Bi Maganga pia aliipongeza BMH kwa kutumia nishati jadidifu katika majiko ya Hospitali na kwamba BMH inatunza mazingira kwa kutokutumia kuni, ambazo zinasababisha mmomonyoko wa udungo and uchafuzi wa mazingira zinapochomwa.

“Tutaitumia BMH kama taasisi ya mfano tunaposhawishi taasisi nyingine kutunza mazingira,” aliongeza Katibu Mkuu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali, Dkt Kessy Shija, alitoa shukrani kwa Katibu Mkuu kwa kuchagua kuitembelea Hospitali ya Benjamin Mkapa na kwamba watakeleza maagizo yake.

“Tutakeleza kwa vitendo maagizo yote ambayo umetupa na tutaendeleza kutunza mazingira eneo la Hospitali,” alisema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa BMH.

BMH imebakia kuwa ndiyo hospitali pekee nchini inayopandikiza figo kwa kutumia wataalamu wake wazawa. Ilianza huduma hii kwa usaidizi wa Shirika la afya la Japan la Tokushukai mwaka 2019. Ilikuwa ni hospitali ya pili nchini kuanzisha huduma hii baada ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Dondoo za Afya na Habari
Kula Mlo Kamili
Kula Mlo Kamili

Eat a combination of different foods, including fruit, vegetables, legumes, nuts and whole grains. A...

  View more
Usivute Sigara
Usivute Sigara

Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mapafu yako, uvutaji wa sigara unaweza sababisha matatizo ya...

  View more
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta

Fats consumed should be less than 30% of your total energy intake. This will help prevent unhealthy...

  View more
Kuendesha Gari.
Kuendesha Gari.

Unashauriwa kutokuendesha gari kila siku na wakati mwingine unatakiwa kutembea walau miguu yako na m...

  View more
Epuka ulevi wa Pombe
Epuka ulevi wa Pombe

There is no safe level for drinking alcohol. Consuming alcohol can lead to health problems such...

  View more