Dkt. CHANDIKA: BIMA YA AFYA KWA WOTE ITAONGEZA WIGO WA HUDUMA
Dkt. CHANDIKA: BIMA YA AFYA KWA WOTE ITAONGEZA WIGO WA HUDUMA

Januari 23, 2023 Dodoma 

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH)-Dodoma, Dkt Alphonce Chandika amesema kuwa Bima ya Afya kwa Wote itaongeza wigo wa huduma na kuwafaidisha wananchi waliyokuwa hawamudu gharama za uchunguzi na matibabu.

Dkt. Chandika aliyasema hayo mwishoni mwa wiki alipokuwa akitoa taarifa katika kikao cha Mkoa wa Dodoma kuhusu mafanikio ya serikali ya wamu ya sita, kilichowahusisha viongozi mbalimbali kuanzia ngazi ya kata hadi Mkoa na kutumia fursa hiyo kutoa wito kwa viongozi hao kushiriki kutoa elimu ya faida Bima ya Afya kwa Wote.

“Bima ya Afya kwa Wote itaongeza wigo wa huduma kwa wananchi, hasa wale waliyokuwa wanashindwa kumudu gharama za uchunguzi na matibabu”Alisisitiza Dkt. Chandika.

Katika hatua nyingine Dkt. Chandika aliishukuru Serikali kwa kusudio lake la kuleta  Bima ya Afya kwa Wote kwa kuwa itaondoa manungúniko na mapungufu mbalimbali yaliyochangiwa na baadhi ya wananchi kushindwa kumudu gharama za matibabu.

Aidha katika kikao hicho, Dkt. Chandika aliwaomba viongozi mbalimbali wakiwe wa dini, wa kiasiasa na wa serikali waliohudhuria kikao hicho kuwahamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote itakapoanza, kwa kufanya hivyo, huduma za Afya zitaboreshwa zaidi utawasaidia wananchi kuwa na uhakika wa matibabu wakati wote.

Dondoo za Afya na Habari
Kula Mlo Kamili
Kula Mlo Kamili

Eat a combination of different foods, including fruit, vegetables, legumes, nuts and whole grains. A...

  View more
Usivute Sigara
Usivute Sigara

Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mapafu yako, uvutaji wa sigara unaweza sababisha matatizo ya...

  View more
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta

Fats consumed should be less than 30% of your total energy intake. This will help prevent unhealthy...

  View more
Kuendesha Gari.
Kuendesha Gari.

Unashauriwa kutokuendesha gari kila siku na wakati mwingine unatakiwa kutembea walau miguu yako na m...

  View more
Epuka ulevi wa Pombe
Epuka ulevi wa Pombe

There is no safe level for drinking alcohol. Consuming alcohol can lead to health problems such...

  View more